Tuesday, September 25, 2012

Papaa On Tuesday......Kama Wengine Wanaweza Kwanini Mimi Nisiweze? | Sam Sasali a.k.a Papaa

Papaa On Tuesday......Kama Wengine Wanaweza Kwanini Mimi Nisiweze? | Sam Sasali a.k.a Papaa

Siku za Papaa on Tuesday ya Samuel Sasali kwangu huwa ni vituko. Imejirudia hii mara kadhaa hebu niseme la leo.
Nilikuwa na mkutano na wadhungu kujadili PhD development yangu. Infact no nimetoka mkutanoni saa hizi. Nimeamka kama saa 3 hivi asubuhi (kwa saa za huko TZ) moja kwa moja kituoni METRO nikadaka 51 ofisini. Nimefika ofisini nikaamua kidogo ninoe kiingereza kwa angalau kupigia simu watu kadhaa. Wakati naanza kufikiri nimpigie nani "Negotiation" ikaanza! Kuna jamaa yuko Norway, hajui kiingereza vizuri, nina rafiki yangu Uingereza, hapatikani kwa simu. Nikawaza kuna Mpare mmoja mji jirani (Mathew) kumbe yuko darasani not reachable. Nikatamni nimpigie papaa (maana kupiga simu huku ni cheap kuliko voda-voda bongo), nikasita maana angeniuliza "Umesoma Papaa yangu ya leo?" Nani anataka maswali magumu. Nikaamua nitafute tu hiyo Ön tuesday" wauu kukuta tu ile Tpic Sentensi ikanikumbusha 2002 naingia chuo kikuu kwa mara ya kwanza walikuja wale jamaa kututisha kuwa hapa chuoni kuna vichwa vitatu (Tundui, Utouh na Mbano) walivyokuwa wanayataja hayo majina wa MU mnakumbuka (siwezi kutaja nimeokoka na nampenda YESU). lakin nilichokumbuka ni tu "kama kuna watu wanapata supp na wengine wanafaulu, mi sijifunzi kwa walioshindwa bali kwa walioshinda" Sasa hiki ndicho kimenifanya nisome makala yote maana ina maudhui tofauti na mlengo wangu wa 2002 na leo ni 2012 (september 25) almost tarehe moja na ile jamaa walikuja kutupa huo umatemate wa mambo ya SUPP. Tarehe 25/09/2002 ilikuwa jumatano na tulikuwa orentation week ndiyo siku nilijipa wazo "Why nijifunze kwa walioshindwa?" Miaka kumi baadaye 25/09/2012 (jumanne), napata wazo jipya "Yaaa nijifunze kwa walioshindwa". Utadhani hili halina maana lakini lina maana tu kwa wenye kuwaza hivi.
1. Aliyenitisha kuhusiana na walioshindwa alikuwa mwanafunzi aliyekuwa mbele yangu mwaka mmoja (alikuwa second na "finalist" year nilikuwa "Fom one")
2. Aliyeleat wazo la kujifunza kwa walioshindwa, ana qualify kuwa "om one" wakati mimi ni "Finalist"
3. Mahusiano ya Mimi "Baba Xtina" na Papaa ni "Mwalimu na Mwanaunzi Pacha" kwa maana, yeye ni mwalimu wangu sasa na siku zote zijazo, lakini ni mwanafunzi wangu wa kwanza "Financial Management"
4. Miongoni mwa wale waliokuja 25/09/2002 pale "BLT" baadaye alikuja kuwa mwanafunzi wangu Masters akifanya M.Sc (AF) ya MU.
5. Nahisi Papaa alitakiwa kuwa mbele yangu MU na hasa ukizingati "Sarakasi" zake za kusoma shule sita kwa miaka minne (kama sikosei)

mwisho: Ufafanuzi. Mzumbe university kuna wanafunzi wa aina zifuatazo na nitalinganisha na mnavyowaita vyuo vingine
1. MU - "Form One" >>> kwingine "First years"
2. MU - "Second year" >> Kwingine "Second year"
3. MU - "Finalist" >>> kwingine "Thid year"
4. MU - "Wazee wa Masters">>> kwingine "Masters"
5. MU - "Viwango DUNI" >>> kwingine "Diploma na Cerificate"
Mwisho wa mwisho, niwatakie siku njema na niwatakie kazi njema. kila jumanne nasoma hii kitu "On tuesday" nilianzishaga yangu "KURUZI" umeme ukawa mgao likazima (Godwin alitabiri kifo chake kabla), Nikaja na "On friday" nikahojiwa "ITADUMU" hahahaha bado ipo, sasa nitakuja na "Reflection on POT" lakini tu Amani Paul Gaseri akimaliza assignment yake!! Popote mkimwona mwambieni.